Thursday , 7 December 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Trump asitisha msaada Palestina
Kimataifa

Trump asitisha msaada Palestina

Donald Trump
Spread the love

DONALD Trump, Rais wa Marekani amesitisha utoaji msaada wa zaidi ya dola 200 milioni kwa Palestina. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Marekani ilipanga kutoa msaada kwa Wapalestina kiasi cha dola 251 milioni, kwa ajili ya kuimarisha utawala bora, afya, elimu na ufadhili wa taasisi za kijamii katika bajeti yake ya mwaka wa fedha wa 2018 ambao unamalizika mwezi Septemba mwaka huu.

Usitishaji huo wa msaada wa Marekani kwa Wapalestina,  umekuja ikiwa imepita miezi kadhaa tangu nchi hiyo kupunguza utoaji misaada kwa Wakala wa Umoja wa Mataifa kwa Wakimbizi wa Palestina (UNRWA).

Mkurugenzi Mkuu wa Marekani jana Ijumaa tarehe 24 Agosti, 2018 alisema Rais Trump ameamuru idara ya serikali kurekebisha  mipango ya ufadhili kwa Benki ya Magharibi na Ukanda wa Gaza.

Mkurugenzi huyo alisema, uamuzi huo umechukuliwa kutokana na changamoto zinazokabili jumuiya za kimataifa katika kutoa misaada kwenye eneo la ukanda wa Gaza. Ambapo kikundi cha wanamgambo cha Hamas kimedhibiti maisha ya raia wa gaza na kudhoofisha hali ya kibinadamu na kiuchumi.

Hata hivyo, hatua hiyo ya Marekani imepingwa vikali na Shirika la Uhuru wa Wapalestina (PLO) likidai kuwa imetumika kama silaha ya kisiasa  na kwamba wapalestina na uongozi wao hawatakuwa na hofu na au kupokea mashinikizo yake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Muandamanaji ajichoma moto akipinga vita Palestina, Israel

Spread the loveMUANDAMANAJI moja ambaye hajafahamika jina, yuko mahututi hospitalini akitetea uhai...

Kimataifa

Urusi kuongeza wanajeshi ikijihami dhidi ya NATO

Spread the loveSERIKALI ya Urusi iko katika mpango wa kuongeza wanajeshi wake,...

Kimataifa

Israel yarejesha mashambulizi Gaza ikilaumu Hamas kukiuka makubaliano

Spread the loveJESHI la Israel, limerejesha mashambulizi katika ukanda wa Gaza, baada...

Kimataifa

Papa Francis kumfukuza Kardinali anayepinga mageuzi Kanisa Katoliki

Spread the loveKIONGOZI wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis, anadaiwa kupanga kumfumkuza...

error: Content is protected !!