Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Moto wateketeza mali za mamilioni Ngara
Habari za SiasaTangulizi

Moto wateketeza mali za mamilioni Ngara

Spread the love

MAGARI matano ya mizigo, yameteketea kwa moto katika kituo cha forodha kilichomo eneo la Rusomo, wilayani Ngara, mpakani mwa Tanzania na Rwanda, leo Jumapili, tarehe 19 Agosti 2018. Anaripoti Mwandishi Wetu kutoka Rusomo … (endelea).

Taarifa kutoka kwa mashuhuda wa tukio hilo zinasema, magari hayo yameteketea kwa moto kufuatia gari moja lililobeba mafuta aina ya petroli kuligonga gari jingine, lililokuwa limeegeshwa katika eneo hilo.

“Ni kweli tukio hilo limetokea kwenye eneo hili. Gari tano ambazo zilikuwa zimeegeshwa kusubiri ruhusa ya kuvuka mpaka, zimeteketea kwa moto,” anasimulia Nyungura Ndyekimana, mfanyabiashara wa Rusomo na raia wa Rwanda.

Anasema, “athari za ajali hii zimekuwa kubwa zaidi kutokana na kukosekana kwa miundo mbinu ya kukaribia na ajali za moto, kama vile gari la zimamoto, ukosefu wa barabara za dharura na kukosekana umakini kwa watu wanaoshughulika na forodha.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!