Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Moto wateketeza mali za mamilioni Ngara
Habari za SiasaTangulizi

Moto wateketeza mali za mamilioni Ngara

Spread the love

MAGARI matano ya mizigo, yameteketea kwa moto katika kituo cha forodha kilichomo eneo la Rusomo, wilayani Ngara, mpakani mwa Tanzania na Rwanda, leo Jumapili, tarehe 19 Agosti 2018. Anaripoti Mwandishi Wetu kutoka Rusomo … (endelea).

Taarifa kutoka kwa mashuhuda wa tukio hilo zinasema, magari hayo yameteketea kwa moto kufuatia gari moja lililobeba mafuta aina ya petroli kuligonga gari jingine, lililokuwa limeegeshwa katika eneo hilo.

“Ni kweli tukio hilo limetokea kwenye eneo hili. Gari tano ambazo zilikuwa zimeegeshwa kusubiri ruhusa ya kuvuka mpaka, zimeteketea kwa moto,” anasimulia Nyungura Ndyekimana, mfanyabiashara wa Rusomo na raia wa Rwanda.

Anasema, “athari za ajali hii zimekuwa kubwa zaidi kutokana na kukosekana kwa miundo mbinu ya kukaribia na ajali za moto, kama vile gari la zimamoto, ukosefu wa barabara za dharura na kukosekana umakini kwa watu wanaoshughulika na forodha.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!