Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Naibu Meya wa Dar atimkia CCM
Habari za Siasa

Naibu Meya wa Dar atimkia CCM

Mussa Kafana, Aliyekuwa Naibu Meya Dar es Salaam
Spread the love

ALIYEKUWA Naibu Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Mussa Kafana amejiuzulu uanachama wa CUF na kuomba kupokelewa ndani ya CCM. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Kafana ambaye pia alikuwa diwani wa kata ya Kiwalani ametangaza kujivua uanachama wa CUF pamoja na kujiuzulu udiwani na unaibu meya wa jiji la Dar es Salaam leo tarehe 18 Agosti, 2018 wakati akizungumza na wanahabari jijini hapa.

Akielezea sababu za kujiuzulu, Kafana amesema mgogoro unaoendelea katika chama hicho unamyima fursa ya kisiasa na hivyo amemaua kuhamia katika chama kisicho na migogoro.

“CUF ina pande mbili zinavutana na mngogoro huu hauwezi kuisha leo wala kesho kwa sababu wanachobishana na kuvutana ni watu wakubwa kwenye chama. Sijaongea na kiongozi yoyote wa CCM na sijajiunga na chama chochote cha siasa ila kama viongozi wa chama hicho wananisikia na watanipokea nitashukuru naomba nipokelewe,” amesema Kafana.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

error: Content is protected !!