Friday , 9 June 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa  BREAKING NEWS: Kofi Annan afariki dunia
Kimataifa

 BREAKING NEWS: Kofi Annan afariki dunia

Hayati Kofi Annan enzi za uhai wake
Spread the love

KATIBU Mkuu wa zamani wa Umoja wa Mataifa (UN) Kofi Annan (80), amefariki dunia asubuhi leo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Taarifa zilizopatikana mchana huu, zinaeleza kuwa Annan, aliyekuwa katibu mkuu wa saba wa umoja huo – kuanzia 1996 hadi 2006, amefariki dunia wakati akipatiwa matibabu nchini Uswisi.

Inaelezwa kuwa Annan, raia wa Ghana, aliugua ghafla – juzi usiku, na hali yake kubadilika jana na kupelekwa katika moja ya hospitali maarufu (haikutajwa) na kufariki saa 11.30 alfajiri.

Annan atakumbukwa zaidi kwa kuhuisha “heshima” ya umoja huo, baada ya kurekebisha baadhi ya miundo na kusimamia utekelezaji wa majukumu yake ipasavyo.

Mwaka 2001, alitunukiwa Tuzo ya Amani ya Nobel (akiwa mshindi sambamba na UN) kwa kile kilichoelezwa kuwa ni “kusimamia Amani ya dunia.” Tuzo za Nobel ni maarufu duniani na hutolewa kwa baadhi ya watu wanaofanya vyema na ipasavyo kusaidia “uhai” wa dunia.

Annan aliyezaliwa Mjini Kumasi, Ghana – Aprili 8, 1938 ameacha mke, Nane na watoto watatu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Kagame afumua tena Jeshi, awafuta kazi maofisa zaidi ya 200 wakiwemo majenerali

Spread the love  RAIS wa Rwanda, Paul Kagame, amewafuta kazi Meja Jenerali...

Kimataifa

Urusi imelipua bwawa kuu la umeme nchini Ukraine

Spread the loveSERIKALI mjini Kyiv nchini, Ukraine imeushutumu utawala wa Rais Vladimir...

Kimataifa

Rais Kagame afanyia mabadiliko makubwa jeshi, usalama wa taifa

Spread the loveRAIS wa Rwanda, Paul Kagame amefanye uteuzi wa wakuu wapya...

Kimataifa

Miili ya waliofariki kwenye ajali ya treni India, kukabidhiwa baada ya vipimo vya DNA

Spread the love  TAKRIBANI watu 260 wamefariki na wengine karibu 650 wamejeruhiwa...

error: Content is protected !!