Friday , 2 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Naibu Meya wa Dar atimkia CCM
Habari za Siasa

Naibu Meya wa Dar atimkia CCM

Mussa Kafana, Aliyekuwa Naibu Meya Dar es Salaam
Spread the love

ALIYEKUWA Naibu Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Mussa Kafana amejiuzulu uanachama wa CUF na kuomba kupokelewa ndani ya CCM. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Kafana ambaye pia alikuwa diwani wa kata ya Kiwalani ametangaza kujivua uanachama wa CUF pamoja na kujiuzulu udiwani na unaibu meya wa jiji la Dar es Salaam leo tarehe 18 Agosti, 2018 wakati akizungumza na wanahabari jijini hapa.

Akielezea sababu za kujiuzulu, Kafana amesema mgogoro unaoendelea katika chama hicho unamyima fursa ya kisiasa na hivyo amemaua kuhamia katika chama kisicho na migogoro.

“CUF ina pande mbili zinavutana na mngogoro huu hauwezi kuisha leo wala kesho kwa sababu wanachobishana na kuvutana ni watu wakubwa kwenye chama. Sijaongea na kiongozi yoyote wa CCM na sijajiunga na chama chochote cha siasa ila kama viongozi wa chama hicho wananisikia na watanipokea nitashukuru naomba nipokelewe,” amesema Kafana.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

Habari za SiasaTangulizi

Zanzibar watangaza rasmi kuwa shamba la Razaba ni mali yao

Spread the love  SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imetangaza rasmi kwamba shamba...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Mwinyi azindua Kamati ya Maridhiano Visiwani

Spread the love  RAIS wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk. Hussein...

error: Content is protected !!