Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Nape Nnauye atoa neno kuhama kwa Mtatiro
Habari za Siasa

Nape Nnauye atoa neno kuhama kwa Mtatiro

Spread the love

NAPE Nnauye, Mbunge wa Jimbo la Mtama ametoa neno baada ya aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi CUF Taifa, Julius Mtatiro kukihama chama hicho, akisema kuwa hamahama hiyo itumike kama fursa ya kujenga upya demokrasia. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Nape ametoa maneno hayo kupitia ukurasa wake wa Twitter, ambapo amesema hamahama hiyo pia itumike kama fursa ya kujenga uimara wa CCM.

Hata hivyo, Nape amesema uimara wa CCM unategemea ubora wa upinzani huku akifananisha na ushindani wa timu za Simba na Yanga.

“Kama msomi wa Sayansi ya siasa, naona hii ni fursa muhimu ya kujengwa kwa aina mpya ya vyama na siasa za upinzani nchini! Kwa demokrasia hamahama hii, ni muhimu itumike kama fursa ya kujenga upya uimara wa CCM unategemea ubora wa upinzani. (Simba/Yanga),” ameandika Nape kupitia ukurasa wake wa Twitter.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!