Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mtatiro aitosa CUF, amuunga mkono Rais Magufuli
Habari za SiasaTangulizi

Mtatiro aitosa CUF, amuunga mkono Rais Magufuli

Spread the love

JULIUS Mtatiro, Aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi ya Chama cha CUF, amejivua uanachama wa chama hicho na kuonesha nia ya kuhamia Chama cha Mapinduzi (CCM). Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Mtatiro ametangaza uamuzi huo leo tarehe 11, Agosti, 2018 mbele ya wanahabari katika mkutano wake uliofanyika kwenye Ukumbi wa Protea jijini Dar es Salaam.

Mtatiro amesema ameamua kuchukua uamuzi huo na kuhamia CCM ili kupata fursa ya kuifanyia nchi maendeleo, akidai kwamba ndani ya CUF aliikosa fursa hiyo.

“Katika tafakari yangu ya kuhama, nilipitia maeneo kama matano ambayo nimefanyia kazi, niliangalia ushiriki na mchango wangu kwenye siasa za CUF, mgogoro unaoendelea kukikumba CUF, eneo la tatu ambalo nimelitafakari kwa upana sana ushiriki wangu kama kijana na kiongozi katika kuchochea maendeleo ya nchi, jambo la nne ajenda ya maendeleo ya nchi, la mwisho ni ustakabali wangu kuhusu masuala ya siasa,” amesema Mtatiro.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!