TUZO ya mwanamke mwenye ushawishi na mhamasishaji zaidi kisiasa Afrika imechukuliwa na Mange Kimambi, raia wa Tanzania. Anaripoti Regina Kelivin … (endelea).
Waandiaaji wa tuzo hiyo wanaotambulika kwa jina la kingereza Black Entertainment Film Fashion Television and Art (BEFFTA) –Burudani, Filamu, Mitindo, Televisheni ya Watu Aweusi wamemchagua Mange kuwa mshindi wa tuzo hiyo dhidi ya wenzake.
Waliokuwa kwenye kinyang’anyiro hicho ni pamoja ni Elie Johson Sirleaf wa Liberia, Joice Majuru kutoka Zimbabwe, Diane Shima Rwigara raia wa Rwanda, Mbali Ntuli kutoka Afrika Kusini na Alengot Oromait kutoka nchini Uganda.
Lengo la BEFFTA ni kuangaza maslahi ya watu weusi katika nchi za Uingereza, Canada, Marekani, Carribbean na nchi za Bara la Afrika.
Awali taarifa za kuwania tuzo hizo zilitolewa na shirika hilo la BFFTA kupitia ukurasa wao unaopatikana kwenye mtandao wa kijamii wa instagram.
Mange amejipatia umaarufu katika mitandao ya kijamii hasa instagram kutokana jumbe zake za ukosoaji kwa viongozi wa serikali na hata viongozi wa dini nchini Tanzania.
Pia aliongeza ‘presha’ zaidi Tanzania kutokana na kutumia mitandao ya kijamii kuhamasisha maandamano aliyopanga kufanyika Aprili 26 mwaka huu.
Hatua hiyo hiyo iliwalazimu viongozi mbalimbali Tanzania kujitokeza na kupinga maandamano hayo yaliyoonekana kushika kasi kupitia mitandao hiyo.
Leave a comment