Sunday , 3 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Mange Kimambi ‘shujaa’ Afrika
Habari MchanganyikoTangulizi

Mange Kimambi ‘shujaa’ Afrika

Mange Kimambi siku aliyofanya maandamano ya kupinga vitendo vinavyofanywa kinyume na haki za binadamu
Spread the love

TUZO ya mwanamke mwenye ushawishi na mhamasishaji zaidi kisiasa Afrika imechukuliwa na Mange Kimambi, raia wa Tanzania. Anaripoti Regina Kelivin … (endelea).

Waandiaaji wa tuzo hiyo wanaotambulika kwa jina la kingereza Black Entertainment Film Fashion Television and Art (BEFFTA) –Burudani, Filamu, Mitindo, Televisheni ya Watu Aweusi wamemchagua Mange kuwa mshindi wa tuzo hiyo dhidi ya wenzake.

Waliokuwa kwenye kinyang’anyiro hicho ni pamoja ni Elie Johson Sirleaf wa Liberia, Joice Majuru kutoka Zimbabwe, Diane Shima Rwigara raia wa Rwanda, Mbali Ntuli kutoka Afrika Kusini na Alengot Oromait kutoka nchini Uganda.

Lengo la BEFFTA ni kuangaza maslahi ya watu weusi katika nchi za Uingereza, Canada, Marekani, Carribbean na nchi za Bara la Afrika.

Awali taarifa za kuwania tuzo hizo zilitolewa na shirika hilo la BFFTA kupitia ukurasa wao unaopatikana kwenye mtandao wa kijamii wa instagram.

Mange amejipatia umaarufu katika mitandao ya kijamii hasa instagram kutokana jumbe zake za ukosoaji kwa viongozi wa serikali na hata viongozi wa dini nchini Tanzania.

Pia aliongeza ‘presha’ zaidi Tanzania kutokana na kutumia mitandao ya kijamii kuhamasisha maandamano aliyopanga kufanyika Aprili 26 mwaka huu.

Hatua hiyo hiyo iliwalazimu viongozi mbalimbali Tanzania kujitokeza na kupinga maandamano hayo yaliyoonekana kushika kasi kupitia mitandao hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

20 wafariki dunia kwa mafuriko Manyara

Spread the loveMVUA za vuli zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali nchini zimeleta madhara...

ElimuHabari Mchanganyiko

CEO NMB awataka vijana kunoa ujuzi wao

Spread the loveAfisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB, Ruth Zaipuna, amewashauri...

Habari Mchanganyiko

TARURA kujenga madaraja 189 kwa teknolojia ya mawe

Spread the loveWakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) imejipanga kujenga...

AfyaHabari Mchanganyiko

Majaliwa aipongeza GGML mapambano dhidi ya Ukimwi

Spread the loveWaziri Mkuu Kassim Majaliwa ameipongeza Kampuni ya Geita Gold Mining...

error: Content is protected !!