Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mkurugenzi Twaweza anyang’anywa ‘Passport’
Habari za SiasaTangulizi

Mkurugenzi Twaweza anyang’anywa ‘Passport’

Aidan Eyekuze, Mkurugenzi Twaweza
Spread the love

MAOFISA wa Uhamiaji wamemnyang’anya Hati ya Kusafiria (passport) Mkurugenzi wa taasisi ya utafiti isiyo ya kiserikali Twaweza Aidan Eyekuze. Anaandika Regina Kelvin … (endelea).

Zitto Kabwe, Kiongozi Mkuu wa ACT-Wazalendo katika ukurasa wake wa twitter ameandika kuwa ‘baada ya wiki kadhaa taasisi hiyo kuchapisha utafiti wake na matokeo kuonesha umaarufu wa rais kushuka. Hati ya kusafiria ya Eyekuze imekuckuliwa na uhamiaji.’

Julai 6, Twaweza ilieleza utafiti wake kwamba, Rais wa Tanzania, Dk. John Magufuli umeshuka kutoka asilimia 96 mwaka 2016 hadi kufikia asilimia 55 mwaka huu.

Na kwamba, asilimia 55 ya wananchi wanaukubali utendaji wa Rais Magufuli tangu alipoingia madarakani mwaka 2015. Kukubalika huko kulipungua kutoka asilimia 96 mwaka 2016, na 71 mwaka 2017.

Kiwango cha kukubalika kwa Rais kimeshuka kutoka kwenye rekodi ya juu kuwahi kuwekwa na Rais wa Tanzania mpaka rekodi ya chini tangu takwimu hizi zianze kukusanywa mwaka 2001.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!