Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mkurugenzi Twaweza anyang’anywa ‘Passport’
Habari za SiasaTangulizi

Mkurugenzi Twaweza anyang’anywa ‘Passport’

Aidan Eyekuze, Mkurugenzi Twaweza
Spread the love

MAOFISA wa Uhamiaji wamemnyang’anya Hati ya Kusafiria (passport) Mkurugenzi wa taasisi ya utafiti isiyo ya kiserikali Twaweza Aidan Eyekuze. Anaandika Regina Kelvin … (endelea).

Zitto Kabwe, Kiongozi Mkuu wa ACT-Wazalendo katika ukurasa wake wa twitter ameandika kuwa ‘baada ya wiki kadhaa taasisi hiyo kuchapisha utafiti wake na matokeo kuonesha umaarufu wa rais kushuka. Hati ya kusafiria ya Eyekuze imekuckuliwa na uhamiaji.’

Julai 6, Twaweza ilieleza utafiti wake kwamba, Rais wa Tanzania, Dk. John Magufuli umeshuka kutoka asilimia 96 mwaka 2016 hadi kufikia asilimia 55 mwaka huu.

Na kwamba, asilimia 55 ya wananchi wanaukubali utendaji wa Rais Magufuli tangu alipoingia madarakani mwaka 2015. Kukubalika huko kulipungua kutoka asilimia 96 mwaka 2016, na 71 mwaka 2017.

Kiwango cha kukubalika kwa Rais kimeshuka kutoka kwenye rekodi ya juu kuwahi kuwekwa na Rais wa Tanzania mpaka rekodi ya chini tangu takwimu hizi zianze kukusanywa mwaka 2001.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!