Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Watekaji waliotumia gari ya UN, wanaswa
Habari MchanganyikoTangulizi

Watekaji waliotumia gari ya UN, wanaswa

Spread the love

JESHI la Polisi Kanda Maluum ya Dar es salaam linawashikilia watu wawili kwa tuhuma za kuteka watu na kudai fedha kwa  kutumia gari yenye namba za Umoja wa Mataifa (UN) ambazo ni T 452 CD 639 Toyota Land Cruiser huku ndani ya gari hilo wakiwa na watu watano waliowateka. Anaripoti Khalifa Abdallah … (endelea).

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amesema watuhumiwa hao ni Hussein Shilingi (30) mkazi wa Kimara Mwisho na Martin Pumba (35) makazi wa Tabata.

Mambosasa amesema baada ya upekuzi ndani ya gari hilo walifanikiwa kukamata vifaa vilivyokuwa vikitumiwa na wahalifu ambavyo ni, redio call moja, pingu jozi tatu, plate namba za magari za mashirika ya serikali, namba za umoja wa mataifa na namba za watu binafsi, kitambulisho cha kughushi chenye nembo ya polisi chenye jina la Martin Pumba.

Vitu vingine walivyokutwa navyo ni pamoja na simu za mikononi za aina mbalimbali, kadi za simu, panga moja, sime mbili, nondo moja, marungu matatu, visu vikuba vinne, maganda matatu ya risasi yanayodhaniwa kuwa ni ya bunduki aina ya SMG, mkasi mkubwa mmoja na karatasi za maelezo ya watu mbalimbali waliokuwa wanawateka pamoja na hirizi mbili.

Mambosasa amesema watuhumiwa  hao walikamatwa tarehe 26 Julai, 2018 maeneo ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam (UDSM) wakiwa na gari yenye namba za umoja wa mataifa (UN) ambazo ni T 452 CD 639 Toyota Land Cruiser huku ndani ya gari hilo wakiwa na watu watano waliowateka.

Jeshi la Polisi lilifanya mahojiano na watu waliotekwa na walieleza kuwa walitekwa katika kipindi cha kuanzia tarehe 23 hadi 25 Julai, 2018 na walikuwa wanatakiwa kutoa Sh. 60 milioni, ambapo watekaji hao walikuwa wanatumia mbinu ya kupiga simu kwa ndugu au jamaa wa waliowateka na kudai fedha hizo ili waweze kuwaachia huru mateka hao.

Inaelezwa kuwa  watuhumiwa hao wamekuwa  wakibadili namba za magari pindi wanaapomaliza kuteka watu ili wasigundulike kwa haraka.

Aidha amesema wanaendelea na mahojiano na watuhumiwa ili kubaini watu wanaoshirikiana nao na watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!