SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Africa (CAF) limetoa majibu ya uchunguzi wa waamuzi wanne wa Tanzania waliofikishwa kwenye Shirikisho hilo kufuatia kuripotiwa kwa vurugu kwenye hoteli waliyofikia nchini Burundi walipokwenda kuchezesha mechi ya Ligi ya Mabingwa Africa Kati ya Rayon ya Rwanda na Lydia Ludica kutoka nchini Burundi. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).
Waamuzi hao ambao ni Soud Idd Lila, Frank John Komba, Mfaume Ali Nasoro na Israel Mujuni walikuwa katika hali ya sintofahamu baada ya kuibuka kwa vurugu kubwa katika hoteli waliofikia kutokana ya madai ya kuwa moja ya timu hizo mbili ilitaka kupanga matokeo kupitia waamuzi hao.
Taarifa iliyotolewa na shirikisho la mpira wa miguu nchni TFF, ilisema CAF, kupitia Katibu wake Mkuu Amr Fahmy ilijilidhisha kuwa hakuna jambo lolote baya lililowazunguka waamuzi hao kuhusiana na mchezo huo uliochezwa tarehe 21 Februari, 2018 katika dimba la Prince Louis Rwagasore, Burundi. Na hivyo wapo safi kuendelea na majukumu yao.
Leave a comment