Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Serikali yawatangazia vita wanaotorosha madini
Habari za Siasa

Serikali yawatangazia vita wanaotorosha madini

Spread the love

SERIKALI imewatangazia vita watu wanaotorosha madini ya Tanzanite pamoja na wanaokwenda kinyume na matakwa ya sheria. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Akizungumza jana tarehe 01 Agosti, 2018 wakati alipofanya ziara ya kutembelea migodi ya madini ya Tanzanite na ukuta wa Mirerani mkoani Manyara, Waziri wa Madini, Angellah Kairuki aliwaonya wezi wa madini hayo kwamba kiama chao kinakuja.

Waziri Kairuki amesema serikali itaendelea kusimamia ulinzi na kudhibiti utoroshwaji wa madini hayo.

“Utoroshaji madini hausaidii, fedha ni za haraka lakini zinawaadhibu watanzania walio wengi kwa kuwa, fedha hizo hizo zingeweza kutumika katika miradi mingine ya maendeleo. Hivyo, kila mtanzania awe mlizi wa mwenzake,” amesema Kairuki.

Kwa upande wake,  Kamishna wa Madini, Mhandisi David Mlabwa, amesema  ni lazima Sheria, Kanuni na taratibu zizingatiwe wakati wa utekelezaji shughuli za uchimbaji madini kwa kuwa serikali inatambua mchango wa kila aina ya madini yanayopatikana nchini.

Naye, Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro, Tumaini Magesa ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Kiteto amesema kuwa, shughuli za uchimbaji katika eneo la Mirerani zinaendelea na hivyo serikali itaendelea kuboresha ulinzi na kuhakikisha kwamba unaimalika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!