Tuesday , 21 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Spika Ndugai apokea barua ya Kalanga kujiuzulu
Habari za SiasaTangulizi

Spika Ndugai apokea barua ya Kalanga kujiuzulu

Job Ndugai
Spread the love

SPIKA wa Bunge, Job Ndugai amepokea barua ya kujivua uanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na kujiuzulu nafasi ya ubunge kwa aliyekuwa  Mbunge Jimbo la  Monduli, Julius Kalanga Laizer. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea). 

Taarifa hiyo ilitolewa jana tarehe 01 Agosti, 2018 na Kitengo cha Habari Elimu kwa Umma na Mawasiliano Ofisi ya Bunge. 

“Kufuatia barua hiyo tayari Mheshimiwa Spika amemuandikia Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Mheshimiwa Jaji Semistocles Kaijage kumfahamisha kuwa Jimbo la Monduli lililoko Mkoani Arusha liko wazi tangu sasa,” ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.

Mheshimiwa Spika ameandika barua hiyo kwa mujibu wa kifungu 37(3) cha Sheria ya Taifa ya Chaguzi (Sura ya 343, ya mwaka 2015)kinachoelekeza kwamba, pale ambapo Mbunge, atajiuzulu, atakufa au sababu nyingine yeyote tofauti na zilizoainishwa katika kifungu cha 113, Spika atamjulisha Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi na kutangaza kwenye Gazeti la Serikali kwamba kiti hicho cha Ubunge kiko wazi.

Taarifa hiyo ilieleza kuwa, kufuatia barua hiyo Tume ya Taifa ya Uchaguzi, inaweza kuendelea na mchakato wa kumpata Mbunge wa kujaza nafasi hiyo iliyowazi ya Jimbo la Monduli.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

M/kiti bodi ya wadhamini Chadema afariki dunia

Spread the loveMWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu

Spread the love  KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe...

error: Content is protected !!