Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Spika Ndugai apokea barua ya Kalanga kujiuzulu
Habari za SiasaTangulizi

Spika Ndugai apokea barua ya Kalanga kujiuzulu

Job Ndugai
Spread the love

SPIKA wa Bunge, Job Ndugai amepokea barua ya kujivua uanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na kujiuzulu nafasi ya ubunge kwa aliyekuwa  Mbunge Jimbo la  Monduli, Julius Kalanga Laizer. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea). 

Taarifa hiyo ilitolewa jana tarehe 01 Agosti, 2018 na Kitengo cha Habari Elimu kwa Umma na Mawasiliano Ofisi ya Bunge. 

“Kufuatia barua hiyo tayari Mheshimiwa Spika amemuandikia Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Mheshimiwa Jaji Semistocles Kaijage kumfahamisha kuwa Jimbo la Monduli lililoko Mkoani Arusha liko wazi tangu sasa,” ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.

Mheshimiwa Spika ameandika barua hiyo kwa mujibu wa kifungu 37(3) cha Sheria ya Taifa ya Chaguzi (Sura ya 343, ya mwaka 2015)kinachoelekeza kwamba, pale ambapo Mbunge, atajiuzulu, atakufa au sababu nyingine yeyote tofauti na zilizoainishwa katika kifungu cha 113, Spika atamjulisha Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi na kutangaza kwenye Gazeti la Serikali kwamba kiti hicho cha Ubunge kiko wazi.

Taarifa hiyo ilieleza kuwa, kufuatia barua hiyo Tume ya Taifa ya Uchaguzi, inaweza kuendelea na mchakato wa kumpata Mbunge wa kujaza nafasi hiyo iliyowazi ya Jimbo la Monduli.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

error: Content is protected !!