Thursday , 9 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa MwanaHALISI huru, kurejea mtaani
Habari za SiasaTangulizi

MwanaHALISI huru, kurejea mtaani

Spread the love

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imeamuru gazeti la kila wiki la MwanaHALISI ambalo lilifungiwa na serikali, liendelee kuchapishwa. Anaripoti Faki Sosi…(endelea). 

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatatu, tarehe 30 Julai, ofisini kwake, Kinondoni, mkurugenzi wa kampuni ya Hali Halisi Publishers Limited (HHPL), Saed Kubenea amesema, mahakama imeridhia MwanaHALISI kurudi tena mtaani, kufuatia mamlaka iliyoifungia kutokuwa na nguvu za kisheria.

MwanaHALISI lilifungiwa na serikali, tarehe 19 Septemba 2017, kwa madai kuwa limekuwa “likiandika habari za uongo, kejeli, upotoshaji, uchochezi na zinazolenga kuwafanya wananchi waichukie serikali yao.”

Hukumu ya kuruhusiwa kuchapishwa kwa MwanaHALISI, imetolewa na Jaji Beatrice Mutungi, tarehe 24 Julai mwaka huu.

Amri ya kufungia MwanaHALISI, ilitolewa na aliyekuwa naibu waziri wa habari, utamaduni, sanaa na michezo, Anastazia Wambura, tarehe 19 Septemba2017.

Kubenea amesema, mahakama imethibisha kuwa gazeti lake, halikuwa na makosa; mkurugenzi wa Idara ya Habari (Maelezo) na naibu waziri Wambura, walijichukulia mamlaka wasiyokuwa nayo.

Amesema, hukumu hiyo imedhihirisha kuwa wapo watendaji ndani ya serikali wanaotumia mamlaka walizopewa “kushughulikia wenzao” kwa maslahi yao binafsi.

Amesema, kutokana na hali hiyo, wanatarajia gazeti hilo kuingiza mtaani Jumatano ya tarehe 8 Agosti na kwamba wamepanga kumchukulia hatua za kisheria Wambura.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

Habari za SiasaTangulizi

Samia: Kuanzia Agosti marufuku kutumia mkaa, kuni

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amemuagiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mwendokasi Kigogo – Segerea kujengwa awamu ya 5

Spread the loveNaibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI), Festo Dugange...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

error: Content is protected !!