Tuesday , 16 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kubenea: Hakuna wa kuning’oa Chadema
Habari za Siasa

Kubenea: Hakuna wa kuning’oa Chadema

Saed Kubenea, Mbunge wa Ubungo
Spread the love

SAED Kubenea, Mbunge wa Ubungo kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) amesema kuwa, hakuna wa kumng’oa ndani ya chama hicho. Anaandika Faki Sosi…(endelea).

Kubenea ametoa kauli hiyo baada ya kuulizwa na waandishi wa habari kuhusu taarifa za kutajwa kutaka kuondoka kwenye chama hicho na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM).

“Hizi taarifa zimeenezwa na baadhi ya watu wakiwemo ndani ya Chadema kwa maslahi wanayoyajua wao na watu hao wanajulikana.

“Mimi niende CCM kwa lipi” amehoji na kuongeza; “mimi bana sitoki Chadema na hakuna wa kunitoa Chadema, nitabaki humo huko,” ameseam Kubenea.

Amesema kuwa, kuhusishwa kwake na kuhama kwa Mwita Waitara aliyekuwa Mbunge wa Ukonga aliyejiunga na CCM wiki iliyopita sio sahihi.

Ameeleza kuwa, hatua ya Mwita kuhamia CCM sio sahihi kwa kuwa wananchi wa Ukonga walimwamini na kumchagua kwa kura nyingi “hivyo alipaswa kupambana akiwa ndani ya Chadema.”

Kubenea amesema kuwa, atapambana ndani ya Chadema na akishindwa ataendelea na kazi yake ya uandishi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Samia arejesha mikopo ya 10%, bilioni 227.96 zatengwa

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amerejesha utaratibu wa utoaji mikopo...

Habari za Siasa

Rais Samia amfariji mjane wa Musa Abdulrahman

Spread the loveRais Samia Suluhu Hassan leo Jumanne amempa pole Mwanakheri Mussa...

Habari za Siasa

Nape: Wanasiasa, wanahabari, wafanyabiashara mteteeni Samia

Spread the loveWaziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano,...

Habari za Siasa

CAG: TAWA imegawa vibali vya uwindaji bila idhini ya waziri

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

error: Content is protected !!