Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe, viongozi Chadema wafutiwa dhamana
Habari za SiasaTangulizi

Mbowe, viongozi Chadema wafutiwa dhamana

Spread the love

MWENYEKITI wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe na viongozi wengine wandamizi wa chama hicho, “wameswekwa rumande,” kwenye kituo cha polisi kati jijini Dar es Salaam. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Taarifa zilizothibitishwa na Casimil Mabina, katibu wa chama hicho Kanda ya Pwani, Mbowe na wenzake wameswekwa rumande, kwa maelekezo ya mkuu wa upelelezi wa Kanda ya Dar es Salaam.

“Muda huu tumeingia kwa Deputy ZCO (naibu mkuu wa upelelezi wa Kanda). Faili analo mmoja wa askari. Dalili zote ni kwamba wanawekwa mahabusu,” anaeleza Mabina katika taarifa yake kwa wanachama wa chama hicho kwenye Kanda hiyo.

Viongozi walioshikiliwa polisi ni pamoja na Mbowe, Katibu Mkuu Dk. Vincent Mashinji, John Mnyika, Salum Mwalim, Peter Msigwa na Ester Matiko.

Mabina anasema, awali kulikuwa na maelekezo ya kuwapeleka mahakama ya Hakim Mkazi Kisutu, ili kijibu tuhuma zinazowakabili.

Katibu huyo amesema wamefutiwa dhamana na mpango kesho watafikishwa mahakamani kujibu mashitaka yao.

Mbowe na viongozi wenzake wanatuhumiwa kuhamamisisha wafuasi wao kufanya maandamano ya tarehe 16 Februari mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!