Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe, viongozi Chadema wafutiwa dhamana
Habari za SiasaTangulizi

Mbowe, viongozi Chadema wafutiwa dhamana

Spread the love

MWENYEKITI wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe na viongozi wengine wandamizi wa chama hicho, “wameswekwa rumande,” kwenye kituo cha polisi kati jijini Dar es Salaam. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Taarifa zilizothibitishwa na Casimil Mabina, katibu wa chama hicho Kanda ya Pwani, Mbowe na wenzake wameswekwa rumande, kwa maelekezo ya mkuu wa upelelezi wa Kanda ya Dar es Salaam.

“Muda huu tumeingia kwa Deputy ZCO (naibu mkuu wa upelelezi wa Kanda). Faili analo mmoja wa askari. Dalili zote ni kwamba wanawekwa mahabusu,” anaeleza Mabina katika taarifa yake kwa wanachama wa chama hicho kwenye Kanda hiyo.

Viongozi walioshikiliwa polisi ni pamoja na Mbowe, Katibu Mkuu Dk. Vincent Mashinji, John Mnyika, Salum Mwalim, Peter Msigwa na Ester Matiko.

Mabina anasema, awali kulikuwa na maelekezo ya kuwapeleka mahakama ya Hakim Mkazi Kisutu, ili kijibu tuhuma zinazowakabili.

Katibu huyo amesema wamefutiwa dhamana na mpango kesho watafikishwa mahakamani kujibu mashitaka yao.

Mbowe na viongozi wenzake wanatuhumiwa kuhamamisisha wafuasi wao kufanya maandamano ya tarehe 16 Februari mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!