Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Nyufa Hostel za Magufuli zaanza kurekebishwa
Habari za Siasa

Nyufa Hostel za Magufuli zaanza kurekebishwa

Spread the love

SIKU chache baada ya kusambaa kwa picha zilizoonesha nyufa katika kuta za majengo ya mabweni ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), nyufa hizo zimeanza kukarabatiwa, anaandika Mwandishi Wetu.

Ukarabati huo unafanyika na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) ambapo Desemba 3, mwaka huu picha za nyufa hizo zilisambaa mitandaoni huku Kumbusho Dawson, Mbunge katika serikali ya wanafunzi UDSM (Daruso) alishikiliwa kuhojiwa na baadaye kuachiwa huru na polisi kitengo cha makosa ya mtandao.

Hata hivyo TBA ilitolea ufafanuzi nyufa hizo kupitia Mtendaji Mkuu wa TBA, Mhandisi Elius Mwakalinga na kueleza kuwa kutokea kwa nyufa hizo ni jambo la kawaida na haina madhara.

Majengo hayo ambayo yalijengwa na TBA ambao wameeleza kuwa bado inaangalia dosari nyingine zilizopo katika majengo hayo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!