Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto Kabwe akubali yaishe matokeo udiwani
Habari za Siasa

Zitto Kabwe akubali yaishe matokeo udiwani

Zitto Kabwe, Kiongozi wa ACT na mbunge wa Kigoma Mjini
Spread the love

BAADA ya kukamilika uchaguzi mdogo wa udiwani katika kata 43 nchini, Kiongozi wa ACT –Wazalendo, Zitto Kabwe amesema chama chake kimekubali kushindwa, anaandika Hamis Mguta.

Katika taarifa aliyoitoa leo, Novemba 27, 2017 Zitto amesema ACT Wazalendo katika uchaguzi wa jana Jumapili Novemba 26, 2017 ilisimamisha wagombea katika kata 17.

“Tumepata matokeo ya kata zote na hakuna kata tuliyoshinda. Wapiga kura wameamua na sisi tumekubali. Tunafanya tathmini ya matokeo nchi nzima na tutazungumza na wananchi. Tunawashukuru kwa kura tulizopata. Tutazienzi kwa kuwa ndiyo haki yetu,” amesema Zitto.

Amesema wanajiandaa kwa uchaguzi mdogo ujao ukiwemo wa ubunge kwenye majimbo yaliyo wazi.
Zitto amesema watatumia mafunzo waliyopata kwenye uchaguzi mdogo  kujipanga kwa uchaguzi ujao.

“Kwetu sisi chama cha ACT Wazalendo, uchaguzi ulikuwa fursa ya kuzungumza na wananchi na kufikisha ujumbe wetu kwa kuwa kuzuiwa mikutano ya hadhara kunatunyima fursa hiyo. Hatutachoka kuendelea kusambaza sera zetu kwa kuwa tunaamini ni bora zaidi na zinazoweza kuleta unafuu kwa wananchi wetu,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

error: Content is protected !!