Tuesday , 5 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto Kabwe akubali yaishe matokeo udiwani
Habari za Siasa

Zitto Kabwe akubali yaishe matokeo udiwani

Zitto Kabwe, Kiongozi wa ACT na mbunge wa Kigoma Mjini
Spread the love

BAADA ya kukamilika uchaguzi mdogo wa udiwani katika kata 43 nchini, Kiongozi wa ACT –Wazalendo, Zitto Kabwe amesema chama chake kimekubali kushindwa, anaandika Hamis Mguta.

Katika taarifa aliyoitoa leo, Novemba 27, 2017 Zitto amesema ACT Wazalendo katika uchaguzi wa jana Jumapili Novemba 26, 2017 ilisimamisha wagombea katika kata 17.

“Tumepata matokeo ya kata zote na hakuna kata tuliyoshinda. Wapiga kura wameamua na sisi tumekubali. Tunafanya tathmini ya matokeo nchi nzima na tutazungumza na wananchi. Tunawashukuru kwa kura tulizopata. Tutazienzi kwa kuwa ndiyo haki yetu,” amesema Zitto.

Amesema wanajiandaa kwa uchaguzi mdogo ujao ukiwemo wa ubunge kwenye majimbo yaliyo wazi.
Zitto amesema watatumia mafunzo waliyopata kwenye uchaguzi mdogo  kujipanga kwa uchaguzi ujao.

“Kwetu sisi chama cha ACT Wazalendo, uchaguzi ulikuwa fursa ya kuzungumza na wananchi na kufikisha ujumbe wetu kwa kuwa kuzuiwa mikutano ya hadhara kunatunyima fursa hiyo. Hatutachoka kuendelea kusambaza sera zetu kwa kuwa tunaamini ni bora zaidi na zinazoweza kuleta unafuu kwa wananchi wetu,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Baba yake Ole Sabaya ashinda Uenyekiti CCM – Arusha

Spread the loveLoy Thomas Sabaya ambaye ni Baba wa aliyekuwa Mkuu wa...

Habari za Siasa

Serikali yaagiza uchunguzi chanzo maporomoko Hanang

Spread the loveSERIKALI imeagiza uchunguzi ufanyike ili kubaini chanzo cha maporomoko ya...

Habari za SiasaTangulizi

Maafa Manyara: Rais Samia akatisha ziara yake Dubai

Spread the loveRAIS wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amekatisha ziara yake...

Habari za SiasaTangulizi

Wataalaam wa miamba watua Hanang

Spread the loveWaziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na...

error: Content is protected !!