Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Wataam watakiwa kumaliza makosa ya mitandaoni
Habari Mchanganyiko

Wataam watakiwa kumaliza makosa ya mitandaoni

Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Atashasta Andikie
Spread the love

WIZARA ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, imewaomba wataalamu wa masomo ya kompyuta kuzingatia mafunzo wanayofundishwa ya mafunzo ya makosa ya mtandao, itasaidia kuondoa migogoro ya watumiaji, anaandika Angel Willium.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, katika uzinduzi wa semina ya mafunzo ya makosa ya mtandao Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Atashasta Andikie, amesema wanatakiwa kuzingatia mafunzo wanayopewa na kufanya kwa vitendo lengo nikutokomeza mashambulizi yanayoendelea mitandaoni.

“Mkutano huu umelenga kuwapa mafunzo wataalamu wa mtandao na kubadilishana uzoefu na mataifa ya Uarabuni, Asia na Afrika,” amesema Andikie.

Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCAR) James Kilaba amesema wanayo madarasa kwa ajili ya wataalamu wajifunze kwa kirefu na wanaendelea kujifunza kwa sababu mara nyingi mambo ya mtandao hubadilika.

Pia Kilaba amesema wanashirikiana na mataifa mbalimbali ili kuweza kuzuia makosa ya mtandao, hivyo tatizo likitokea siyo lazima liletwe kwenye ofisi zao, hata nchi nyingine inaweza kutatua na wana vifaa vya kutosha ambavyo vinaboreshwa kutokana na kubadilika kwa matumizi ya mtandao.

Semina ya mafunzo ya makosa ya mtandao yanafanyika kila mwaka, yalianza 2014 wataalamu wa mtandaoni upewa mafunzo na kisha wanajifunza wenyewe kwa vitendo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!