Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Undani wa kinachoendelea Zimbabwe huu hapa
Kimataifa

Undani wa kinachoendelea Zimbabwe huu hapa

Spread the love

KUMEKUWA na sintofahamu ya kile kinachoendelea nchini Zimbabwe huku kukiwa na taarifa tofauti ya mapinduzi yaliyofanyika nchini humo dhidi ya Rais Robert Mugabe na mgogoro ndani chama chake cha Zanu PF.

Hii hapa matukio yanaoendelea nchini humo na undani wa mgogoro huo

Magari ya kijeshi katika mitaa ya Harare

Magari ya kijeshi yanaonekana yakipiga doria katika barabara za mji mkuu wa Zimbabwe Harare. Mapema leo magari ya kijeshi na wanajeshi, wakionekana kuelekeza au kuzuia magari.

Emmerson Mnangagwa ni nani?

Akaunti ya chama cha Zanu PF inasemama kuwa Emmerson Mnangagwa amefanywa kuwa rais wa mpito. Mnangawa mwenye umri wa miaka 75 alifukuzwa kazi ya Makamu wa rais kutokana na kile serikali ilisema kuwa kutokuwa mtiifu.

Kufutwa kwake kulionekana kama nia ya kumwezesha mke wa Rais Mugabe, Grace, kufuata nyayo za mumewe na kuwa kiongozi wa Zimbabwe.

Awali alikuwa ametoa wito kwa mumewe kumfuta makamu wa rais. Mnangagwa ambaye ni mku wa zamani wa ujasusi amekuwa mtu ambaye alitarajiwa kumrithi Rais Mugabe 93.

Kufutwa kwake kulimaanisha kuwa Grace Mugabe anatarajiwa kuteuliwa kuwa makamu wa rais wakati wa mkutano maalum wa chama tawala cha Zanu-PF mwezi ujao.

Mugabe anajiandaa kuondoka madarakani

Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe anajiandaa kuondoka madarakani saa chache baada ya jeshi la Zimbabwe kutwaa madaraka, kwa mujibu wa mtandao maarufu wa habari nchini Afrika Kusini.

“Mugabe anajiandaa kuondoka madarakani,” mtandao wa wa News24 uliandika bila ya kutoa taarifa zaidi.

Misukusuko ya kisiasa imekuwa ikiongezeka tangu Mugabe hivi majuzi amfute Emmerson Mnangagwa, mshirika wake wa miaka mingi kama makamu wa Rais.

Mzozo wa Zimbabwe

Jeshi la Zimbabwe lilisoma taarifa kwenye kituo cha runinga cha serikali ZBC, likisema kuwa linachukua hatua ya kuwalenga wahalifu.

Hata hivyo limesema kuwa hayo sio mapinduzi ya kijeshi na Rais Mugabe yuko salama. Milio mikubwa ya risasi ilisikika katika maeneo ya kaskazini mwa mji mkuu Harare mapema leo.

Taarifa hiyo ya jeshi ilikuja saa kadhaa baada ya jeshi kudhibiti kituo cha ZBC.

Mwanamume mmoja ambaye alikuwa amevaa sare za jeshi alisema kuwa jeshi linataka kukabiliana na watu ambao wanatenda uhalifu unaoleta madhara ya kijamii na kiuchumi nchini Zimbabwe.

“Wakati tutakapomalzia wajibu wetu, tunatarajia kuwa hali itadudi kuwa sawa.” Taarifa hiyo ilisema kuwa Mugabe 93, na familia yake wako salama.

Haijulikani ni nani anaongoza hatua hiyo ya kijeshi. Magari ya wanajeshi waliojihami kwa silaha yanaonekana maeneo ya mjini Harare.

Hali hiyo ya wasi wasi wa lolote kuweza kutokea, imeanza hapo jana jioni, ambapo wanajeshi wakiwa na silaha walionekana wakijipanga katika maeneo kadhaa pamoja na kuzingira ofisi za shirika la utangazaji la Zimbabwe ZBC.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!