Friday , 2 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Hukumu ya Sheikh Ponda kizungumkuti
Habari za Siasa

Hukumu ya Sheikh Ponda kizungumkuti

Sheikh Ponda Issa Ponda
Spread the love

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam imeshindwa kutoa hukumu ya rufaa ya Serikali dhidi ya Sheikh Issa Ponda kwa mara nyingine, anaandika Faki Sosi.

Katika rufaa hiyo Serikali inapinga hukumu ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro iliyomuachia huru Sheikh Ponda katika tuhuma ya uchochezi.

Hukumu hiyo iliyotarajiwa kutolewa jana na Jaji Mkasi Mongwa ambaye amesema ameshindwa kutoa hukumu hiyo kwa kuwa hajamaliza kuianda na badala yake ataitoa Novemba 23, mwaka huu.

Inatarajiwa kwenye hukumu hiyo endapo Jaji Mongwa anayesikiliza shauri hilo ataridhika na madai ya upande wa Serikali, Sheikh Ponda atatiwa hatiani na kuhukumiwa adhabu.

Kama Jaji hataona ukweli katika madai ya Serikali, atatupilia mbali rufaa hiyo na kumuachia huru Sheikh Ponda.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

Habari za SiasaTangulizi

Zanzibar watangaza rasmi kuwa shamba la Razaba ni mali yao

Spread the love  SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imetangaza rasmi kwamba shamba...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Mwinyi azindua Kamati ya Maridhiano Visiwani

Spread the love  RAIS wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk. Hussein...

error: Content is protected !!