Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Takukuru waingia kazini ‘issue’ ya Nyalandu
Habari za Siasa

Takukuru waingia kazini ‘issue’ ya Nyalandu

Naibu Mkurugenzi wa Takukuru, Brigedia Jenerali
Spread the love

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), imesema kuwa suala la aliyekuwa Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu imelisikia na imeanza kulifanyia kazi, anaandika Angel Willium.

Takukuru wameingia kazini kulifanyia kazi shutuma za Nyalandu baada ya kutuhumiwa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla, alipokuwa anachangia Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa mwaka 207/2018 na kuiagiza taasisi hiyo na polisi kumchunguza Nyalandu.

Naibu Mkurugenzi wa Takukuru, Brigedia Jenerali, John Mbungo amesema wamesikia tuhuma za Nyalandu na wameanza kuzichunguza na wakimkuta na hatia watamfikisha kunakostahili.

Mbugo ameitoa kauli hiyo leo ikiwa ni siku moja baada ya Waziri Dk. Kigwangala kumlipua Nyalandu akimtuhumu kwa matumizi mabaya ya madaraka.

Dk. Kigwangala amesema Nyalandu aliikosesha serikali mapato ya Sh. 32 bilioni kwa miaka miwili aliyohudumu katika wizara hiyo kwa kushindwa kusaini sheria ya tozo kwa hoteli za kitalii.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Mpina mwiba CCM, ahofia kuzibwa mdomo

Spread the loveWAKATI Chama cha Mapinduzi (CCM), kikijinasibu kuwa kinara wa demokrasia...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Mabeyo ametuepusha

Spread the loveNIMEGUSWA na uadilifu, utiifu na uaminifu wa Mkuu mstaafu wa...

Habari za SiasaTangulizi

CCM yaitaka TAKUKURU kuichunguza Chadema tuhuma alizoibua Lissu

Spread the loveCHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimeitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana...

error: Content is protected !!