Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Takukuru waingia kazini ‘issue’ ya Nyalandu
Habari za Siasa

Takukuru waingia kazini ‘issue’ ya Nyalandu

Naibu Mkurugenzi wa Takukuru, Brigedia Jenerali
Spread the love

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), imesema kuwa suala la aliyekuwa Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu imelisikia na imeanza kulifanyia kazi, anaandika Angel Willium.

Takukuru wameingia kazini kulifanyia kazi shutuma za Nyalandu baada ya kutuhumiwa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla, alipokuwa anachangia Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa mwaka 207/2018 na kuiagiza taasisi hiyo na polisi kumchunguza Nyalandu.

Naibu Mkurugenzi wa Takukuru, Brigedia Jenerali, John Mbungo amesema wamesikia tuhuma za Nyalandu na wameanza kuzichunguza na wakimkuta na hatia watamfikisha kunakostahili.

Mbugo ameitoa kauli hiyo leo ikiwa ni siku moja baada ya Waziri Dk. Kigwangala kumlipua Nyalandu akimtuhumu kwa matumizi mabaya ya madaraka.

Dk. Kigwangala amesema Nyalandu aliikosesha serikali mapato ya Sh. 32 bilioni kwa miaka miwili aliyohudumu katika wizara hiyo kwa kushindwa kusaini sheria ya tozo kwa hoteli za kitalii.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!