Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Dk. Shika aendelea kusota, Polisi kumpima akili
Habari Mchanganyiko

Dk. Shika aendelea kusota, Polisi kumpima akili

Spread the love

KAIMU Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Benedict Kitalika amesema jeshi la polisi linaendelea kummshikilia Dk. Louis Shika kwa kuwa bado linaendelea na uchunguzi huku wakijipanga kumfanyia vipimo vya akili, anaandika Angel Willium.

Kitalika amesema mtuhumiwa huyo atafikishwa mahakamani muda wowote baada ya uchunguzi kukamilika, lakini hadi sasa hakuna ndugu yake yeyote aliyejitokeza kushirikiana na jeshi la polisi katika uchunguzi unaoendelea.

Kamanda amesema kabla ya kumfikisha mahakamani jeshi la polisi linawasiliana na mamlaka nyingine za serikali kuangalia kama kuna uwezekano wa kumpima Dk. Shika kama ana matatizo ya akili.

Dk Shika anatuhumiwa kwa kuvuruga mnada wa nyumba za bilionea Said Lugumi ulioendeshwa na kampuni ya udalali ya Yono Auction Mart baada ya kushindwa kulipa asilimia 25 ya malipo ya awali ya gharama za nyumba hizo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari Mchanganyiko

Chongolo aonya viongozi vijiji kutouza NIDA kwa wageni

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amewaonya viongozi wa...

error: Content is protected !!