Wednesday , 27 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Dk. Shika aendelea kusota, Polisi kumpima akili
Habari Mchanganyiko

Dk. Shika aendelea kusota, Polisi kumpima akili

Spread the love

KAIMU Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Benedict Kitalika amesema jeshi la polisi linaendelea kummshikilia Dk. Louis Shika kwa kuwa bado linaendelea na uchunguzi huku wakijipanga kumfanyia vipimo vya akili, anaandika Angel Willium.

Kitalika amesema mtuhumiwa huyo atafikishwa mahakamani muda wowote baada ya uchunguzi kukamilika, lakini hadi sasa hakuna ndugu yake yeyote aliyejitokeza kushirikiana na jeshi la polisi katika uchunguzi unaoendelea.

Kamanda amesema kabla ya kumfikisha mahakamani jeshi la polisi linawasiliana na mamlaka nyingine za serikali kuangalia kama kuna uwezekano wa kumpima Dk. Shika kama ana matatizo ya akili.

Dk Shika anatuhumiwa kwa kuvuruga mnada wa nyumba za bilionea Said Lugumi ulioendeshwa na kampuni ya udalali ya Yono Auction Mart baada ya kushindwa kulipa asilimia 25 ya malipo ya awali ya gharama za nyumba hizo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari Mchanganyiko

Wizara ya madini kurusha ndege ya utafiti wa madini Geita

Spread the loveKutokana na mchango wa wachimbaji wadogo wa madini kwenye pato...

Habari Mchanganyiko

Jafo aagiza kampuni za madini kuzingatia utunzaji mazingira, azitaka zijifunze kwa GGML

Spread the loveWAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia apewa tano ujenzi barabara Mtwara

Spread the loveWANANCHI wa Mkoa wa Mtwara, wameishukuru Serikali ya Rais Dk....

error: Content is protected !!