Saturday , 2 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema yaanza kumsulubu Nyalandu
Habari za SiasaTangulizi

Chadema yaanza kumsulubu Nyalandu

Lazaro Nyalandu, aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii. Picha ndogo waziri wa sasa wa wizara hiyo, Dk. Hamisi Kigwangalla
Spread the love

SIKU chache baada ya aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu kujivua uanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na nafasi yake ya ubunge na kujiunga na Chadema, ameanza kuonja chungu ya uamuzi wake, baada kushutumiwa kwa matumizi mabaya ya madaraka, anaandika Dany Tibason.

Shutuma hizo dhidi ya Nyalandu zimeibuliwa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamis Kigwangalla bungeni leo alipokuwa akichangia Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa mwaka 207/2018.

Dk Kigwangalla ameiagiza Takukuru na polisi kumchunguza Nyalandu kwa matumizi mabaya ya madaraka ili sheria ichukue mkondo wake.

Waziri huyo amesema Nyalandu alipokuwa waziri aliikosesha serikali mapato ya Sh. 32 bilioni kwa miaka miwili aliyohudumu katika wizara hiyo kwa kushindwa kusaini sheria ya tozo kwa hoteli za kitalii.

Mbali na tuhuma hiyo, pia alimtuhumu kutumia helkopta ya mwekezaji mmoja raia wa kigeni, kipindi cha kampeni zake za kugombea urais 2015, wakati kampuni ya raia huyo ilikuwa ikituhumiwa kwa ujangili.

Nyalandu aliwahi kuliliwa akisema kuwa tuhuma ambazo zimeanza kuibuliwa mitandao dhidi yake si za kweli bali zinalenga tu kumchafua na kuhoji iweje ziibuliwe sasa zaidi ya miaka miwili tangu aachie uwaziri.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Mwalimu jela miaka mitatu kwa rushwa

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mfawidhi, wilaya ya Igunga, mkoani Tabora imemhukumu...

Habari za Siasa

Rais Samia kuzindua programu ya nishati safi ya kupikia kwa wanawake Afrika

Spread the loveRais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuzindua programu ya...

Habari za Siasa

AG aiagiza kamati ya maadili kuwashughulikia mawakili wanaokiuka maadili

Spread the loveMWANASHERIA Mkuu wa Serikali (AG), Dk. Eliezer Feleshi, ameagiza Kamati...

Habari za Siasa

Jaji avunja ukimya sakata la Mpoki kusimamishwa uwakili

Spread the loveJAJI Mkuu wa Tanzania, Prof. Ibrahim Juma, amekitaka Chama cha...

error: Content is protected !!