Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Wakandarasi wazawa waililia serikali
Habari Mchanganyiko

Wakandarasi wazawa waililia serikali

Ujenzi reli ya kisasa
Spread the love

VYAMA vya wakandarasi vya Contractors Association of Tanzania, Tanzania Civic Engineering Contractors na Association of Citizen Contractors, wameiomba serikali iendelee kutoa fursa za kazi kwenye ujenzi wa miundombinu nchini, anaandika Angel Willium.

Wakandarasi hao wameiomba serikali kupata kazi ya kujenga miundombinu kama reli, nishati, bomba la kusafirisha mafuta, ujenzi wa Makao Makuu ya Dodoma na sekta ya maji kwa wakandarasi wazawa.

Mwenyekiti wa Vyama vya Wakandarasi, Injinia Lawrence Mwakyambiki amesema hayo wakati akitambulisha siku ya wakandarasi ambayo itakayofanyika kila mwaka, kuwa wakipewa kazi hizo pesa watakazopata zitatumika kuinua uchumi ndani ya nchi.

“Wakandarasi wa hapa nchini wanaweza kukuza uchumi wa kwa sababu pesa wanazopata katika ujenzi zitasaidia kujenga hoteli au shule nchini kwetu,’’ amesema Injinia Mwakyambiki.

Injinia Mwakyambiki amesema lengo ya kuwa na siku ya wakandarasi ni kubadilishana uzoefu katika utendaji wa miradi mbalimbali na kutoa fursa kwa washiriki 200-300.

Aidha Injinia Mwakyambili amesema wanawashukuru wadau wa wakandarasi wakiwemo Commercial Bank of Afrika (CBA) na NMB Bank na wafadhili wengine kwa kuendelae kufanya kazi na wakandarasi wazawa.

Siku ya wakandarasi imepangwa kufanyika Novemba 17, mwaka huu katika Ukumbi wa Diamond Jubilee, jijini Das es Salaam na itakuwa ikifanyika tarehe hiyo kila mwaka.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari Mchanganyiko

Chongolo aonya viongozi vijiji kutouza NIDA kwa wageni

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amewaonya viongozi wa...

error: Content is protected !!