Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wakandarasi wazawa waililia serikali
Habari Mchanganyiko

Wakandarasi wazawa waililia serikali

Ujenzi reli ya kisasa
Spread the love

VYAMA vya wakandarasi vya Contractors Association of Tanzania, Tanzania Civic Engineering Contractors na Association of Citizen Contractors, wameiomba serikali iendelee kutoa fursa za kazi kwenye ujenzi wa miundombinu nchini, anaandika Angel Willium.

Wakandarasi hao wameiomba serikali kupata kazi ya kujenga miundombinu kama reli, nishati, bomba la kusafirisha mafuta, ujenzi wa Makao Makuu ya Dodoma na sekta ya maji kwa wakandarasi wazawa.

Mwenyekiti wa Vyama vya Wakandarasi, Injinia Lawrence Mwakyambiki amesema hayo wakati akitambulisha siku ya wakandarasi ambayo itakayofanyika kila mwaka, kuwa wakipewa kazi hizo pesa watakazopata zitatumika kuinua uchumi ndani ya nchi.

“Wakandarasi wa hapa nchini wanaweza kukuza uchumi wa kwa sababu pesa wanazopata katika ujenzi zitasaidia kujenga hoteli au shule nchini kwetu,’’ amesema Injinia Mwakyambiki.

Injinia Mwakyambiki amesema lengo ya kuwa na siku ya wakandarasi ni kubadilishana uzoefu katika utendaji wa miradi mbalimbali na kutoa fursa kwa washiriki 200-300.

Aidha Injinia Mwakyambili amesema wanawashukuru wadau wa wakandarasi wakiwemo Commercial Bank of Afrika (CBA) na NMB Bank na wafadhili wengine kwa kuendelae kufanya kazi na wakandarasi wazawa.

Siku ya wakandarasi imepangwa kufanyika Novemba 17, mwaka huu katika Ukumbi wa Diamond Jubilee, jijini Das es Salaam na itakuwa ikifanyika tarehe hiyo kila mwaka.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!