Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mzungu kortini kwa kukutwa na fuvu la Nyumbu.
Habari Mchanganyiko

Mzungu kortini kwa kukutwa na fuvu la Nyumbu.

Nyundo ya Hakimu
Spread the love

RAIA wa  Denmark Ricki Thomson (49), amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam  kwa kosa ka kukutwa fuvu la Nyumbu., Anaandika Faki Sosi.

Mtuhumiwa huyo amekutwa na fuvu hilo bila kibari cha Mkurugenzi wa wanyama pori nchini.

Mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo,  Cyprian Mkeha, Wakili wa Serikali Kishenyi Mutalemwa akiwa amedai  kuwa tukio hilo lilitokea Oktoba 9, mwaka huu katika Uwanja Ndege wa Kimataifa Julius Nyerere bila kuwa na kibali.

“Ulikamatwa na fuvu hilo bila kuwa na kibali kutoka kwa Mkurugenzi wa wanyama pori nchini,” amedai Kishenyi.

Baada ya kusomewa mashtaka hayo mtuhumiwa amekana na upande wa Jamhuri umedai kukamilisha upelelezi
Kesi hiyo imeahirishwa hadi Oktoba 16, mwaka huu itakapokuja kutajwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!