Wednesday , 8 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Waziri Kairuki akumbuka vyeti feki
Habari za Siasa

Waziri Kairuki akumbuka vyeti feki

Angela Kairuki, Waziri wa Madini
Spread the love

ALIYEKUWA  Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, Angela Kairuki leo ameaga  ofisi yake ya zamani huku akikumbuka alivyohangaika na watumishi waliokuwa na vyeti feki. anaandika Angel Willium.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Kairuki amesema katika kipindi cha miezi 23 tangu ateuliwa kuongoza wizara hiyo, amekumbana na changomoto nyingi.

Amesema suala la vyeti feki ambalo liliwakumba watumishi wa serikali wapatao 12,000 ulikuwa ni mtihani mkubwa kwake wakati akiongoza wizara hiyo ambayo ipo chini ya Rais.

“Baadhi ya maofisa utumishi hawakuwa waaminifu walikuwa wanawaficha wale wenye feki,  lakini suala hilo tulilikamilisha kwa kiasi kikubwa,’’ amesema

Kwa upande wake, Waziri mpya wa wizara hiyo, George  Mkuchika ameahidi kuendeleza kasi na nidhamu kwa watumishi wa umma.

Kairuki ameteuliwa kuwa Waziri wa Madini kumrithi mtangulizi wake, George Simbachawene ambaye alitimuliwa kazi kutokana na kutajwa katika ripoti ya Bunge iliyochunguza madini ya Almasi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

Habari za SiasaTangulizi

Samia: Kuanzia Agosti marufuku kutumia mkaa, kuni

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amemuagiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mwendokasi Kigogo – Segerea kujengwa awamu ya 5

Spread the loveNaibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI), Festo Dugange...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

error: Content is protected !!