Tuesday , 26 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema wamtaka IGP Sirro kufunga ‘domo’
Habari za SiasaTangulizi

Chadema wamtaka IGP Sirro kufunga ‘domo’

Simon Sirro, Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania (IGP)
Spread the love

CHAMA  cha Demokrasia na Maendeleo  (Chadema), kimemtaka Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini ( IGP),  Simon  Sirro kuacha kutoa vitisho kwa wananchi na wanasiasa kwa kuwataka waache kuzungumzia tukio la Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema),  (Tundu Lissu kupigwa risasi 38 mkoani Dodoma kwa kuwa hiyo siyo kazi yake, anaandika Mwandishi wetu.
Chadema wamesema hakuna sheria yoyote inayompa Sirro mamlaka hayo na kwamba anatakiwa kuacha kutoa kauli za kuwanyamazisha.

Kauli hiyo ya Chadema, imetolewa leo na Mwanasheria wa chama hicho, John Mallya  alipozungumza na waandishi wa habari makao makuu ya chama hicho.

Amesema Sirro hana ubavu wa kuzuia watu wakiwamo wanasiasa kuendelea kujadili suala hilo.

“Ibara ya 18 ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatoa haki na fursa kwa wananchi kutoa maoni na mawazo yao na kupashana habari pamoja na sheria nyingine na  ibara hii ndio msingi, ” amesema Malya.

Aidha,  ameeleza kuwa Sirro anaongozwa na sheria kubwa ya jeshi la polisi na huduma saidizi ambayo inatoa maelezo ya nani anaweza kumuamuru, na kuwa na mamlaka ya kuamuru askari wake na siyo  raia wa kawaida.

“IGP anyamaze andelee na upelelezi, msisikilize Sirro anachoeleza hamvunji sheria kwa kujadili nani amejaribu kumuua Tundu Lissu, msiingilie upelelezi wao sawa, msiwazuie kufanya upelelezi  sawa lakini jadilini,” amesema.

TAZAMA VIDEO HAPO CHINI

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia avunja bodi ya REA

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua Balozi Jacob Kingu, kuwa...

Habari za SiasaTangulizi

Chande aliyeng’olewa TANESCO kwenda TTCL apelekwa Posta

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua aliyekuwa, Mkurugenzi Mkuu wa...

Habari za Siasa

Kamugisha aanika utekelezaji mpango kazi 2022/23

Spread the loveMWENYEKITI wa Ngome ya Vijana ya Chama Cha ACT-Wazalendo Mkoa...

Habari za Siasa

Vijana ACT-Wazalendo wakabidhiwa kivumbi kulinda kura uchaguzi 2024,2025

Spread the loveNGOME ya Vijana ya Chama cha  ACT-Wazalendo, imetakiwa kuwanoa wafuasi...

error: Content is protected !!