Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Waziri Kairuki akumbuka vyeti feki
Habari za Siasa

Waziri Kairuki akumbuka vyeti feki

Angela Kairuki, Waziri wa Madini
Spread the love

ALIYEKUWA  Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, Angela Kairuki leo ameaga  ofisi yake ya zamani huku akikumbuka alivyohangaika na watumishi waliokuwa na vyeti feki. anaandika Angel Willium.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Kairuki amesema katika kipindi cha miezi 23 tangu ateuliwa kuongoza wizara hiyo, amekumbana na changomoto nyingi.

Amesema suala la vyeti feki ambalo liliwakumba watumishi wa serikali wapatao 12,000 ulikuwa ni mtihani mkubwa kwake wakati akiongoza wizara hiyo ambayo ipo chini ya Rais.

“Baadhi ya maofisa utumishi hawakuwa waaminifu walikuwa wanawaficha wale wenye feki,  lakini suala hilo tulilikamilisha kwa kiasi kikubwa,’’ amesema

Kwa upande wake, Waziri mpya wa wizara hiyo, George  Mkuchika ameahidi kuendeleza kasi na nidhamu kwa watumishi wa umma.

Kairuki ameteuliwa kuwa Waziri wa Madini kumrithi mtangulizi wake, George Simbachawene ambaye alitimuliwa kazi kutokana na kutajwa katika ripoti ya Bunge iliyochunguza madini ya Almasi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!