Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Michezo Edwin achomoka na milioni 60 tatu mzuka
Michezo

Edwin achomoka na milioni 60 tatu mzuka

Mshindi wa mchezo wa bahati nasibu ya Tatu, Mzuka Edwin Kawito wa Dodoma
Spread the love

EDWIN Kawito(25), mkazi wa Manispaa ya Dodoma amekabidhiwa Sh. milioni 60 alizojishindia katika droo ya 10 ya mchezo wa bahati nasibu ya tatu mzuka, anaandika Dany Tibason.

Zawadi hiyo ilikabidhiwa kwa Kawito na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Christina Mndeme. Kawito aliibuka mshindi wa mchezo wa bahati nasibu ya tatu mzuka katika droo ya 10.

Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa fedha hizo, Kawito, amesema hatazitumia fedha hizo kwa sasa mpaka kwanza apate ushauri wa wataalam jinsi ya kuzitumia fedha hizo.

Amesema amekuwa akicheza mchezo huo mara kwa mara tangu ulipoanza hapa nchini. Ameongeza kuwa amekuwa akicheza mara moja hadi mbili katika juma huku akieleza kwamba katika kipindi cha nyuma aliwahi kufanikiwa kushinda hadi Sh. 300,000.

“Nilikuwa nikicheza na rafiki zangu lakini kuna kipindi nilitaka kukata tama, rafiki zangu walinihamasisha niendelea kucheza wakieleza kuwa nimewahi kushinda nyuma katika droo za saa ukilinganishwa wao,”amesema

Kwa upande wake, Mndeme alimpongeza mshindi huyo na kuishukuru tatu mzuka kwa kufika mkoani Dodoma huku akiwataka Watanzania kucheza mchezo huo.

“Ninayo furaha kuona mshindi wa tatu mzuka kwa kipindi hiki anatokea Dodoma, tunayo imani kubwa kuwa mshindi atabadilisha maisha yake na ya familia yake pamoja na jamii inayomzunguka,” amesema.

Tatu mzuka imefanikiwa kutoa zaidi zinazofikia shilingili bilioni mbili tangu ilipoanzishwa Agosti mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

Michezo

Beti na Meridianbet mechi za leo

Spread the love IKIWA leo hii ni Jumapili tulivu kabisa, Meridianbet wanamkwambia...

error: Content is protected !!