Saturday , 4 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Uchaguzi  wavuruga UVCCM Mwanza 
Habari za Siasa

Uchaguzi  wavuruga UVCCM Mwanza 

Umoja wa Vijana CCM (UVCCM)
Spread the love

UCHAGUZI wa marudio wa kumtafuta mwenyekiti mpya wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi CCM (UVCCM), katika wilaya ya Nyamagana jijini Dar es Salaam zimegubikwa vurugu, anaandika Hamis Mguta.

Vurugu hizo vimeibuka baada ya wajumbe kutoka Kata ya Mahina kuzuiwa kuingia ukumbini kupiga kura kwa madai ya kuwa si wajumbe halali.

Katibu wa wajumbe hao, Samora Msiba amesema baada ya kuhoji sababu ya wao kuzuiwa kuingia ukumbini walielezwa kiongozi wao wa kata hana mawasiliano au mahusiano mazuri na serikali.

“Tunaomba viongozi wa ngazi za juu waliangalie suala hili kwa kuwa hata sisi tuna haki ya kupiga kura na si kusukumwa na kususiwa ovyo kwa kuhusishwa na kesi zisizotuhusu,” amesema Msiba.

Hata hivyo, chanzo chetu kinaeleza kuwa vurugu zimesababisha walinzi wa chama hicho (Green Guard) kuzuiwa kufanya kazi yao na badala yake mgambo wa Jiji la Mwanza kusimamia uchaguzi huo.

Kuhusu kuzuiliwa kwa walinzi hao wa Green Guard, Mwenyekiti wa UVCCM Kata ya Mahina ambaye pia ni Katibu wa Green Guard wilayani humo Kagambo Paul amesema amekerwa na kitendo cha kuporwa jukumu lake la kusimamia uchaguzi na kupewa jeshi la akiba la mgambo.

Uchaguzi kwa mara ya kwanza ulifanyika Septemba 23 ambao mshindi hakupatikana kutokana na kura kutofikia nusu ya zilizopigwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mbatia ambwaga Selasini, mahakama yaamuru alipwe fidia

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuamuru...

Habari za SiasaTangulizi

Mkulo afariki dunia, kuzikwa kesho Kilosa

Spread the loveALIYEKUWA Waziri wa Fedha na Mbunge wa Kilosa (CCM), Mustafa...

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

error: Content is protected !!