Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kesi ya Mdee kumtusi Magufuli yapigwa kalenda
Habari za Siasa

Kesi ya Mdee kumtusi Magufuli yapigwa kalenda

Halima Mdee (mwenye nguo nyeupe) akiwa mahakamani akisubiri kesi yake kutajwa kabla ya kuhairishwa
Spread the love

KESI inayomkabili mbunge wa Kawe, Halima Mdee (Chadema), imepigwa kalenda hadi Oktoba 11,mwaka huu itakapoanza kusikilizwa, anaandika Hellen Sisya.

Mdee ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), anakabiliwa na kesi ya kutoa lugha ya matusi dhidi ya Rais John Magufuli.

Anadaiwa kutoa maneno hayo mwezi July mwaka huu, akiwa katika makao makuu ya chama hicho yaliyopo katika mtaa wa Ufipa, Kinondoni jijini Dar es salaam.

Kesi hiyo inasikilizwa na Hakimu Victoria Nongwa wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam na anatetewa na mawakili watatu wakiongozwa na Wakili msomi Peter Kibatala huku upande wa Jamhuri ukiwakilishwa na mawakili wawili wakiongozwa na wakili msomi, Mutalemwa Kishenyi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

error: Content is protected !!