Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Huduma za Mkemia Mkuu zafika mikoani
Habari Mchanganyiko

Huduma za Mkemia Mkuu zafika mikoani

Mkemia Mkuu wa Serikali, Prof. Samwel Manyele
Spread the love

MAMLAKA ya Mkemia Mkuu wa Serikali imelenga kuimarisha utendaji kazi wa maabara  katika kanda zake za Nyanda za juu kusini, na kanda ya ziwa kwa kuzipatia vifaa vya kisasa, anaandika Irene Emmanuel.

Akiongea na waandishi wa habari, Cletus Mnzava, Kaimu Meneja Masoko, Mawasiliano na Huduma kwa Wateja amesema lengo kuu katika kuimarisha shughuli za maabara ni kufanya uchunguzi maalum za kisayansi huko huko mikoani badala ya kuja Dar es Salaam.

Amesema wamejenga majengo ya kudumu ili kuwekeza vifaa vya kudumu tofauti na ilivyokuwa hapo awali.

“Ujenzi wa majengo hayo umeanza kwa baadhi ya kanda kama vile Nyanda za juu kusini amabapo jingo letu linatarajiwa kukamilika mwaka huu wa fedha, lipo eneo la Iwambi Mbeya, Arusha lipo Maeneo ya Mount Meru,” amesema Mnzava.

Miradi hiyo ya kuimarisha Maabara za Kanda inaendelea kutekelezwa kutokana na uelekezaji wa fedha zinazopatikana kwa ajili ya kuimarisha zaidi utoaji wa huduma za maabara kwa wananchi.

Mamlaka hiyo imevitaka vyombo vya habari kusaidia katika kufikisha ujumbe kwa wanajamii kuendelea kutumia huduma za Maabara ambazo zimesogezwa karibu zaidi na wanajamii katika Mikoa ya Mbeya, Katavi, Songwe, Rukwa, Lindi, Mtwara, Songea, Dar es Salaam, Pwani, Dodoma, Singida, Dodoma, Morogoro, Tabora, Iringa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari Mchanganyiko

Chongolo aonya viongozi vijiji kutouza NIDA kwa wageni

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amewaonya viongozi wa...

Habari Mchanganyiko

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu wa GGML

Spread the loveSHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) pamoja na Wakala...

error: Content is protected !!