Tuesday , 23 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Waziri Nchemba aridhia wakimbizi kurudi kwao
Habari Mchanganyiko

Waziri Nchemba aridhia wakimbizi kurudi kwao

Spread the love

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba amesema serikali ya Tanzania haifukuzi wakimbizi kama inavyodaiwa, anaandika Hamisi Mguta.

Mwigulu amesema hayo katika kikao cha kuweka maandalizi ya kuwarejesha wakimbizi raia wa Burundi ambao walioomba kwa ridhaa yao kurudi nchini kwao.

“Serikali ya Tanzania haifukuzi wakimbizi, tunaunga mkono hiari yao ya kuondoka, wenyewe kwa kuwa waliishinikiza serikali kwa kufanya fujo ili walirudishwe kwao na mimi kama waziri mwenye dhamana niliwaambia sitaongeza polisi kupambana na watu wanaotaka kurudi kwao,” amesema.

Amesema kuwa Tanzania inaendelea na majukumu yake yaliyobainishwa kwenye mikataba ya kimataifa ya kupokea na kutunza wakimbizi na mpaka sasa Tanzania ina Wakimbizi zaidi ya 351,400 kutoka Burundi na Kongo.

“Wakimbizi 73,000 wanatoka Kongo na 277,535 wanatoka Burundi. na 150 ni wabantu kutoka Somalia na 338 ni wa kutoka mataifa mengine,”amesema.

Aidha, ameeleza kuwa sheria za kimataifa zinaelekeza kwamba kama watu watajiandikisha kwa ridhaa yao kwamba wanataka kurudi walipotoka na wana uhakika kuwa sababu iliyowafanya wakimbie haipo tena.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari Mchanganyiko

DC ampongeza Dk. Rose Rwakatare kwa kusaidia waathirika wa mafuriko Mlimba

Spread the loveMWENYEKITI wa Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk.  Rose Rwakatare...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!