Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Huduma za Mkemia Mkuu zafika mikoani
Habari Mchanganyiko

Huduma za Mkemia Mkuu zafika mikoani

Mkemia Mkuu wa Serikali, Prof. Samwel Manyele
Spread the love

MAMLAKA ya Mkemia Mkuu wa Serikali imelenga kuimarisha utendaji kazi wa maabara  katika kanda zake za Nyanda za juu kusini, na kanda ya ziwa kwa kuzipatia vifaa vya kisasa, anaandika Irene Emmanuel.

Akiongea na waandishi wa habari, Cletus Mnzava, Kaimu Meneja Masoko, Mawasiliano na Huduma kwa Wateja amesema lengo kuu katika kuimarisha shughuli za maabara ni kufanya uchunguzi maalum za kisayansi huko huko mikoani badala ya kuja Dar es Salaam.

Amesema wamejenga majengo ya kudumu ili kuwekeza vifaa vya kudumu tofauti na ilivyokuwa hapo awali.

“Ujenzi wa majengo hayo umeanza kwa baadhi ya kanda kama vile Nyanda za juu kusini amabapo jingo letu linatarajiwa kukamilika mwaka huu wa fedha, lipo eneo la Iwambi Mbeya, Arusha lipo Maeneo ya Mount Meru,” amesema Mnzava.

Miradi hiyo ya kuimarisha Maabara za Kanda inaendelea kutekelezwa kutokana na uelekezaji wa fedha zinazopatikana kwa ajili ya kuimarisha zaidi utoaji wa huduma za maabara kwa wananchi.

Mamlaka hiyo imevitaka vyombo vya habari kusaidia katika kufikisha ujumbe kwa wanajamii kuendelea kutumia huduma za Maabara ambazo zimesogezwa karibu zaidi na wanajamii katika Mikoa ya Mbeya, Katavi, Songwe, Rukwa, Lindi, Mtwara, Songea, Dar es Salaam, Pwani, Dodoma, Singida, Dodoma, Morogoro, Tabora, Iringa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!