Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge Chadema atinga uraiani
Habari za Siasa

Mbunge Chadema atinga uraiani

Wabunge Ester Bulaya na Halima Mdee
Spread the love

HATIMAYE mbunge wa Bunda (Chadema), Ester Bulaya amepata dhamana baada ya kushikiliwa na Polisi kanda maalum ya Tarime na Rorya kwa amri ya Mkuu wa wilaya ya hiyo Glorious Luoga, anaandika Mwandishi Wetu.

Kabla ya kupata dhamana leo hii, wanachama wa Chadema kutoka maeneo mbalimbali mkoani Mara ikiwamo jimboni kwake, walifurika kituo cha polisi.

Kutokana na wingi wa wananchi hao wakiongozwa na Mbunge wa Tarime vijijini, John Heche, polisi wameonekana kuweka ulinzi mkali.

mwishoni mwa wiki, Bulaya alikamatwa na jeshi la Polisi akiwa katika Hotel ya Kifa Best Point Wilayani Tarime akidaiwa kujiandaa kutaka kufanya mkusanyiko kinyume cha sheria.

Kamanda wa polisi Tarime/Rorya Kamishina Msaidizi Mwandamizi Henry Mwaibambe alisema Bulaya hakutakiwa kushiriki katika mkutano wa Ester Matiko (Chadema), ambaye ni mbunge wa Tarime mjini

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!