SERIKALI imesema asilimia 75 ya wananchi jijini Dar es Salaam wamejenga katika maeneo holela ambayo hajapimwa, anaandika Mwandishi wetu.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi na kwamba zoezi la upimaji ardhi litafanyika nchi nzima.
Amesema hadi kufikia mwaka 2020 wawe wamemaliza zoezi la kurasimisha ardhi kwa wananchi na kuwapatia hati.
Lukuvi amesema kilaa kipande cha ardhi kitapimwa na kwamba hakuna mtu atakayemiliki sehemu ambayo haijapimwa.
Waziri huyo alikuwa akizungumza katika kituo cha Luninga cha Azam na amesema wameanza kupima katika mkoa wa Morogoro.
Leave a comment