Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Walioshikilia Bombadier wamlima barua JPM
Habari za SiasaTangulizi

Walioshikilia Bombadier wamlima barua JPM

Spread the love

KAMPUNI ya mawakili nchini Canada – Irving Mitchell Kilichman (IMK) – imemlima barua Rais John Magufuli, iliyosheheni masharti mazito ya kuachiwa ndege yake aina ya Bombadier Q400, anaandika Saed Kubenea.

Taarifa kutoka Ikulu, jijini Dar es Salaam, wizara ya mambo ya nje na ubalozi wa Tanzania nchini Canada zinasema, IMK imechukua hatua hiyo, kufuatia maelekezo iliyopewa na kampuni ya Stirling Civil Engineering Ltd (SCEL) ya nchini humo.

SCEL inadai serikali ya Tanzania kiasi cha dola za Marekani 38.7 milioni (Sh. 87 bilioni), kufuatia kuvunjwa kwa mkataba wake wa ujenzi wa barabara ya Dar es Salaam hadi Bagamoyo, miaka 13 iliyopita.

Katika barau hiyo, SCEL inasema, haitaachia ndege ya Tanzania inayoishikilia mpaka serikali ilipe kwanza dola milioni 12.5 (sawa na bilioni 27.8) kati ya dola 38.7 inazopaswa kulipa.

Aidha, SCEL inasema, haitaachia ndege hiyo mpaka Rais Magufuli na serikali yake, watakapokubali kwa maandishi, kulipa kiasi kingine cha dola za Marekani 25.5 milioni.

Habari kamili juu ya taarifa hiyo, soma gazeti la MwanaHALISI la leo (Jumatatu).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

error: Content is protected !!