Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Serikali yajibu mapigo ya Mbowe
Habari Mchanganyiko

Serikali yajibu mapigo ya Mbowe

Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO,Hassan Abbasi
Spread the love

HATIMAYE  hoja zilizotolewa na Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) zimemuibua msemaji wa serikali wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Hassan Abbas, anaandika Catherine Kayombo.

Abbas ameibuka leo mchana na kusisitiza kwamba uchumi wa Tanzania bado uko imara tofauti na ilivyosemwa na Chadema kupitia mwenyekiti wake Freeman Mbowe, alipokutana na wanahabari kueleza maazimio ya kikao cha kamati kuu ya chama hicho  kilichofanyika tarehe 29-30 Julai jijini Dar es Salaam.

Mbowe aliyataja maeneo yanayoyumbisha uchumi wa nchi kuwa ni pamoja na mwenendo wa mikopo katika sekta binafsi, ongezeko la deni la taifa na kushuka kwa mzunguko wa fedha kusababisha kuathiri biashara.

Akizungumza na wanahabari, Abbas amesema, uchumi wa upo vizuri ukilinganisha mataifa mengine barani Afrika, kwa miaka mitatu mfululizo bado uko katika ukuaji usiopungua asilimia 7.0 hadi 7.2.

Amesema ukuaji wa uchumi unaizidi Rwanda ambayo inakua kwa  6%, Uganda 5% na Kenya 6.4%.

Amesisitiza kuwa uimara wa uchumi wa nchi ni namna ya  kudhibitiwa kwa mfumuko wa bei, kuendelea kuvutia uwekezaji na utekelezaji wa miradi mikubwa.

Amewataka wananchi kuchapa kazi kwa bidii ili kujiletea maendeleo bila kutegemea nguvu ya serikali.

 

 

 

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!