Tuesday , 30 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Majaliwa apigia debe uwekezaji nchini
Habari Mchanganyiko

Majaliwa apigia debe uwekezaji nchini

Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania
Spread the love

WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa ametembelea kiwanda cha kampuni ya SBC Tanzania Ltd kinachotengeneza vinywaji baridi pamoja na kiwanda cha kukata na kung’arisha mawe ya asili (mabo) cha Marmo Granito Mines Tanzania Ltd, vilivyoko katika eneo la Iyunga Mjini Mbeya, anaandika Mwandishi Wetu.

Amevitembelea viwanda hivyo kwa lengo la kukagua utekelezaji wa sera ya kujenga uchumi wa viwanda nchini, ambao ndiyo kipaumbe cha Serikali ya Awamu ya Tano.

Majaliwa alivitembelea viwanda hivyo akiwa katika ziara yake ya kikazi mkoani Mbeya.
Akiwa katika kiwanda cha Pepsi, alikagua maendeleo ya ujenzi wa upanuzi na wa kiwanda hicho kwa ajili ya kuanza uzalishaji wa vinywanji baridi kwenye chupa za plastiki.

Alishauri kampuni hiyo kuendelea kupanua uwekezaji wake hapa nchini kwa kuwa Tanzania ina sera na mazingira mazuri ya uwekezaji.

Kiwanda hicho kilijengwa mwaka 1999 kikiwa na wafanyakazi 75 na kwa sasa kina wafanyakazi 190.

“Nawashauri muendelee kuwekeza Tanzania kwani mbali na utulivu wa kisiasa pia sera na mazingira yake ya uwekezaji ni mazuri.” amesema

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

7 wafa Ulanga, mbunge alia kutelekezwa na mawaziri, Tanroad

Spread the loveWatoto saba wamepoteza maisha na zaidi ya kaya 70 kukosa...

Habari Mchanganyiko

Bil 12.4 zimetumika ujenzi wa miradi wilaya ya Momba

Spread the love MKUU wa wilaya ya Momba mkoani Songwe Kennan Kihongosi...

AfyaHabari Mchanganyiko

Songwe katika mikakati ya elimu ya lishe kudhibiti udumavu

Spread the love  SERIKALI mkoani Songwe imejipanga kuendelea kutoa elimu ya lishe...

Habari Mchanganyiko

NBC yapata tuzo ya mwezeshaji bora wa mikopo serikali Afrika

Spread the loveBenki ya NBC imepata tuzo ya Mwezeshaji Bora wa Pamoja...

error: Content is protected !!