Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Waziri Mavunde awatua ndoo wananchi Mhande
Habari Mchanganyiko

Waziri Mavunde awatua ndoo wananchi Mhande

Mhe. Anthony Mavunde (MB), Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu Wenye Ulemavu
Spread the love

MKUU wa Wilaya ya Dodoma Mjini Christina Mndeme amezindua mradi wa maji katika kijiji cha Mhande huku akiwaonya watakaoharibu miundombinu ya mradi huo watachukuliwa hatua za kisheria, anaandika Mwandishi Wetu.

Mradi huo umefadhiliwa na Shirika la Wamishionari wa Damu Takatifu ya Yesu(CPPS), kutokana na maombi ya Mbunge wa Dodoma mjini, Anthony Mavunde.

Hatua hiyo ya Mavunde ilitokana na wananchi hao kukabiliwa na kero ya maji kwa muda mrefu hali iliyowalazimu kutembea zaidi ya kilomita 15 kufuata maji kijiji cha Ntyuka.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Mndeme alilishukuru shirika hilo kwa ufadhili wa mradi huo na kumpongeza Mavunde kwa kuwa mstari wa mbele kutatua kero za wanachi wake hususani maji katika kata ya Ngh’ongh’ona.

Amesema hatasita kuwachukulia hatua watu watakaoharibu miundombinu ya mradi huo wa maji kwa kuwa kumekuwepo na watu wenye nia mbaya ya kuhujumu miundombinu.

“Mwili unahitaji maji unapotafuta maji mbali roho inasononeka hata muda wa kusali unaukosa, tunashukuru sana shirika hili lakini wananchi tuna wajibu wa kuutunza mradi huu ambao ni wa thamani kubwa sana hapa tumeambiwa umegharimu kiasi cha Sh. milioni 35,” amesema

Aliwataka wananchi hao kila mmoja kuwa mlinzi wa mwenzie ili mradi huo uweze kudumu kwa muda mrefu na kuwasisitiza maji hao yatumike kwa malengo yaliyokusudiwa.

“Sasa changamoto hii ya maji imetatuliwa ninachowaomba wananchi wa Mhande mfanye kazi kwa bidii ili kujiletea maendeleo kwa kuwa awali mlipoteza muda mwingi kutafuta maji,” amesema

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!